Pages

Ads 468x60px

Tuesday, July 23, 2013

Katiba Mpya: Wajumbe Mikoani Watoa Maoni Mabaraza ya Katiba

Wajumbe wa Baraza la Katiba la Halmshauri ya Wilaya ya Iramba Mkoani Singida wakiwa katika majadiliano ya kuipitia Rasimu ya Katiba Mpya iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo hivi karibuni.
Mjumbe wa Baraza la Katiba la Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe Mkoani Kagera, Bw. Frederick Kabendwe akwasilisha maoni ya Wajumbe hao kuhusu Rasimu ya Katiba Mpya iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika mkutano uliofanyika Wilayani humo hivi karibuni.
Mjumbe wa Baraza la Katiba la Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Mkoani Shinyanga, Bi Caroline Shayo akitoa maoni yake kuhusu Rasimu ya Katiba Mpya katika eneo la kuhusu Maadili ya Viongozi wa Umma katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo hivi karibuni.
Mjumbe wa Baraza la Katiba la Halmshauri ya Wilaya ya Moshi Mkoani Kilimanjaro, Bi. Jackline Moshi akichangia hoja wakati wa mkutano wa kuijadili Rasimu ya Katiba Mpya iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika Mkutano uliofanyika jana katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo.
Mjumbe wa Baraza la Katiba la Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Mkoani Rukwa Bw. Charles Wakuling’anga akiwasilisha maoni ya kundi lake lililojadili eneo la haki za Binadamu katika Rasimu ya Katiba Mpya iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika mkutano uliofanyika katika Halmashauri hiyo hivi karibuni. 
chanzo : issa michuzi
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:

Post a Comment